Sunday, January 5, 2014

IWAPO KUMEIBUKA HOJA YA KUWEPO KWA SERIKALI MBILI ,AMBAPO WANANCHI WENGI WANATAKA KUWEPO NA SERIKALI TATU NA HASA VIJANA WALIYOKO KWENYE VYUO MBALIMBALI, JE SERIKALI IMEJIANDAAJE KUWAELIMISHA UZURI WA KUWA NA SERIKALI MBILI NA UBAYA WA KUWA NA SERIKALI TATU?




Maswali kadhaa yanaulizwa na watu kuhusu masuala ya kuwepo   kwa Serikali mbili au tatu,na kuna vuta ni kuvute katika hoja hiyo kwa wananchi , ambapo wengi wao hasa vijana wengi wanataka kuwepo kwa Serikali tatu na ni kitu ambacho kinatarajiwa kuwepo kwenye Katiba ya Nchi.

 Sasa iwapo inatokea  kutoka kwa baadhi ya wananchi wachache wenye hoja ya kuwepo kwa Serikali mbili,wakati wengi wao wanahitaji kuwepo na Serikali tatu na hasa wasomi vijana katika vyuo vya elimu ya juu nchini.
   Ni nini unadhani kitatokea baada ya kutangaziwa hivyo? Na je iwapo itatokea hivyo Serikali imejiandaaje kutuliza au kuwaelimisha watu hao ambao wengi wao wamechoka kuwa na Serikali mbili na wanadai Serikali tatu bila kujali athari zake baadaye “ liwalo na liwe itajulikana mbele kwa mbele”
   Jambo hilo siyo la mzaha wala si la kulichukulia juu juu,kwa kuwa vijana wetu wengi bila kujali wasomi ama si wasomi,wavijijini au wa mjini wote wamekuwa na kauli moja.Hivyo Tume ya katiba iliangalie kwa macho mawili matokeo ya Hoja hiyo,na namna gani watalikabili suala hilo iwapo litatokea.Hatupendi litokee.


No comments:

Post a Comment