Wednesday, October 21, 2015

WAKATI ZIMEBAKIA SIKU TATU WATANZANIA WATUMIE HAKI YAO YA KUCHAGUA VIONGOZI WANAO WATAKA MKURUGENZI WA HUDUMA ZA SHERIA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI BWANA EMANNUEL KAVISHE ASEMA MWENYE KUTANGAZA MATOKEO NI TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

Aidha Bw. Kavishe amesema Viongozi wa Vyama na wananchi wanatakiwa kupiga kura zao kwa amani na utulivu na kwamba ,baada ya kupiga kura watu warudi walikotoka na kusubili matokeo ambayo yatangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Amesema Mtu atayepata kura nyingi atatangazwa kutoka kwenye chama chochote ambacho mgombea amepata kura nyingi.
kuhusu idadi kamili ya wapiga kura tarehe 25 mwezi huu ,amesema kuwa ni watu milioni 22..7 ambao wanatarajiwa katika upigaji kura siku hiyo,nakwamba kila mtu atapiga  kura kwenye kituo alichojiandikisha,na kama yuko nje ya kituo chake basi mtu huyo atakuwa amekosa haki yake ya kumchagua kiongozi anaye mtaka.
Pia kasema ili kuepusha vurugu zisizo na sababu wananchi wafuate maelekezo ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi,na kuheshimu Katiba.Na madai ya kubaki kwenye vituo baada ya kupiga kura, inamaana mawakala waliyowekwa na vyama vyao hawaviamini.maana waele ndiyo watao hakikisha mgombea wake amepata kura ngapi.

Saturday, October 17, 2015

WANAFUNZI 177 WA CHUO CHA UHASIBU CBM DODOMA KILICHOJULIKANA KAMA ASEK WAMEHITIMU KATIKA NGAZI YA STASHAHADA NA CHETI











Wahitimu hao wa 177 wakiwemo 102  wa Stashahada  na 75 wa Cheti katika fani za Procurement and Supply,Marketing,Banking and Financial and Accountancy  katika Chuo hicho jana 

Saturday, October 10, 2015

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAKAYA KIKWETE AZINDUA KIWANDA CHA KUCHAKATA GESI MADIMBA MTWARA LEO

Nakwamba Rais amezindua viwanda vingine  vya Mtwara kikiwemo cha saruji,kiwanda kikubwa ambacho kitawanufaisha wananchi wa Kusini na majirani zao.

Tuesday, October 6, 2015

BLOG YA TUJIFUNZE KUSINI INATOA POLE KWA FAMILIA YA MWANASIASA MKONGWE MCHUNGAJI CHRISTOPHER MTIKILA ,PAMOJA NA WANASIASA KWA KUFUATIA KIFO CHA MWANA SIASA HUYO AMBAPO MCHANGO WAKE UILIKUWA BADO UNAHITAJIKA

Tukio la mwana siasa huyo limemshitua kila mmoja wetu , lakini hatuna uwezo zaidi wa kuamua lini na wapi na muda gani binadamu atatoweka duniani  na kwa mtindo gani,yote tumuachie Mungu kwani yeye ndiye mwenye kujua nani anamuhitaji kumchukua.
Hivyo Familia na wale wote wenye mapenzi mema kwa marehemu Mtikila kuwa na subira hasa kwa kipindi chote cha msiba huu,kwani Bwana alitoa na Bwana alichukua.Roho ya Marehemu Mungu ailaze mahali pema peponi Amina.

WAKATI ZIMEBAKI SIKU CHAHCE KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA MADIWANI,WAGUNGE NA URAIS,WATANZANIA WAMETAKIWA KUWA KUTUNZA SHAHADA ZAO ZAKUPIGIA KURA

Baadhi ya wananchi wenye kuipenda amani utulivu,pamoja na utulivu, upendo kwa atanzania wote kuacha kuwahadaa watu  wenye shahada zao za kupigia kura kuzifanya ziwe bidhaa kwa mafaniko yao katika kuchaguzi ujao.

 Aidha wanaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kusikiliza Sera za wagombea mbalimbali wa vyama vyote ,ili wajue na wachambue mbivu na mbicha tarehe 25 mwezi huu.

Lakini sanasana cha muhimu ni kuaandaa mazingira ya Amani ,utulivu siku hiyo ya kupiga kura.Hasa kila mmoja amalizapo kufanya kitendo cha haki yake ya kumchagua Diwani,Mbunge na Rais tarehe 25, arudi nyumbani kwakwe kusubili matokeo.

Wale ambao wanatarajia kubakia vituoni kusubiri kuona aliyemchagua kashinda,waache kwani kufanya hivyo kutasababisha uvunjifu wa Amani.Nini maada ya mawakala wa vyama na Tume ya Uchaguzi,Kazi ya kutangaza matokeo ni Tume ya Uchaguzi wengine Turudi majumbani mwetu.

Inajulikana kuwa kura ni siri ya mpiga kura,sasa wewe mwingine kushabikia fulani lazima ashinde je wewe ulikuwa na wapigakura wote nchini ukaona wamemchagua huyo unaye sisitita kuwa kashinda ,jamani tuwaachie wenyewe watakao hesabu kura na kutoa matangazo.

Blogu hii imesikiliza maoni ya baadhi ya Wananchi wa Dodoma wakielezea mtazamo wao katika mwelekeo wa Uchaguzi mkuu tarehe 25 mwezi huu,na kwamba iwapo wananchi watafuata maelekezo ya Tume ya Uchaguzi na Vyombo vya Ulinzi na Usalama ,Uchaguzi siku hiyo utakuwa wa  Amani na Utulivu kwani Tanzania ni Kisiwa cha Amani.Hivyo tumuombe Mungu aifanye siku hiyo iwe ya Amani na Utulivu na Atuongoze katika kuwapata viongozi ambao ni chaguo lake.

Saturday, September 19, 2015

WASHABIKI ACHENI TABIA ZA KUCHANA MABANGO YA WAGOMBEA NAFASI MBALIMBALI ZA UONGOZI KATIKA UCHAGUZI MKUU UJAO HIVI PUNDE MWAKA HUU

Blogu hii imekuta baadhi ya wananchi katika Manispaa ya Dodoma wakilaani vikali kitendo cha kuchaniwa bango la mgombea ubunge wa Jimbo la Dodoma mjini kupitia CCM hivi karibuni nyakati za usiku,na kwamba kitendo hicho hakikuwapendezesha watu wenye hekima na busara zao mjini hapa.
.
Wanasema vitendo hivyo havina tija wala faida kwao na pengine watu hao hawajui thamani za vitu.Wanajiuliza walikuwa na tatizo gani na bango mpaka kulichana, wamesema mambo ya uchaguzi ni ya mpito tu baada ya hapo hali itaendelea kama kawaida,sasa aliyefanya kitendo hicho anapokutana na mgombea huyo atakuwa na amani moyoni mwake.

Aidha walisema vitendo hivyo havifai kama ndiyo ushabiki wa aina hiyo basi haufai kwakuwa ni vitendo vinavyo ashiria uvunjifu wa amani na upendo. katika Jamii ya Kitanzania na Duniani kote

Kufuatia kauli ya viongozi wa ngazi ya juu wa ulinzi na usalama wa mkoa huu,kwamba la kumtaka kila mwananchi akisha piga kura siku hiyo arudi nyumbani kwake kusubili matokeo,Kauli hiyo kwa watu kama hao inaweza kugonga mwamba kwa kutaka kubakia vituoni kusubiri matokeo.

Alisema watu  watakao kiuka agizo hilo asishangae kuona vyombo vya usalama vitapo mshughulikia kikamilifu maana atakuwa ameyataka mwenyewe kwa sababu ya ushabiki,hawajui ushabiki una weza kusababisha machafuko ya kupigwa na hata vifo vya kujitakia.Hivyo wenye tabia kama hizo waziache maana zita waletea wananchi kukosa amani kwa ajili ya watu wachache wasiye taka kusikia.

Tuesday, September 1, 2015

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAKAYA MRISHO KIKWETE AAGWA NA VYOMBO VYA ULINZI NA USALMA KATIKA UKUMBI WA DIAMOND JUBILEE JIJINI DAR ES SALAM


Ameagwa na vyombo vya ulinzi na Usalama Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam na kupewa zawadi ya Trector na majembe yake ambapo Mama Salma Kikwete  amepewa zawadi ya ng’ombe wa maziwa.
Katika hotuba yake na vyombo hivo amewashukuru sana,kasha akasema anaondoka ikiwa watu bado wanampenda.
Aidha alisema anauhakika kuwa vyombo vya Ulinzi na usalama vipo katika hali nzuri, vikiwa na zana za kivita  imara, kujenga  Air Force imengwa,nyumba 10000 zinajengwa  ikiwa nyumba 6,000 ni Askari wa kawaida ambapo nyumba 4,000 ni za Mofisa wa ngazi za juu ,wakati na chini.
Jesha la polisi wanaletewa magari ambapo mipango imesha fanyika Nchini India,magari hayo muda wowote yatawafikia Jeshi la Polisi.
Magereza wao bado kupanga mapendekezo yao,amewaambia wafanye haraka kabla hajaondoka aidhinishe ili atakaye mpokea amkabidhi.
Alisema alichofarijika nalo ni la Umoja wa vyombo vya Ulinzi na Usalama,Kuboresha maslahi ya watumishi wa Umma na Vyombo vya Usalama.
Usipo wekeza kwenye vyombo vya ulinzi na Usalama ,Unaweka rehani maisha ya wananchi,pamoja na ughali wake lazima kuwekeza kwenye vyombo vya Ulinzi na usalama kwa usalama wa ulinzi wan chi na watu wake.
Kama vyomba ulinzi na usalama ni dhaifu mali zote zitahujumiwa bila kujua.Meli mbili zimeanza kulinda kwenye bahari yenye kina kirefu.
Uimara wa uchumi wan chi lazima ulindwe na Jeshi lake na uchumi ule lazima ulindwe kwa upanga.msipowekeza kwenye ulinzi na usalama ,mabenki yote yataibiwa kila siku.
Alisema Dunia sasa inabadilika kwa Sayansi na Teknolojia,lazima na majeshi yetu yafikie huko,Mf moi kumenunuliwa mashine yenye thamani ya Dollar milioni 2, ili kuokoq mqisha ya wananchi ,ukiogopa aghali huwezi kuokoa maisha ya wanachi.
Aidha alisema mwaka huu kuna uchaguzi,vyombo vya ulinzi na usalama hasa Polisi,kuhakikisha upigwaji kura unakuwa wa usalama ,hategemei kuwa kutakuwa na matukio ya kulishinda jeshi la Polisi.
Anastaafu atarudi  kuwa raia maarufu, Hawezi kwenda kuomba atoe ushauri kwa Rais,maana Rais washauri wake. Akitaka ushauri ataenda kuomba ushauri wa kulima mananasi yake,alisema Duniani hapa amefanya kazi kubwa ya Urais.siwezi kuomba kazi,kwa manufaa ya nchi yake kama ataombwa ushauri nitakuwa tayari.
Amesema kuwa walikuwa ndiyo nguzo yake,mhimili wake,kama walivyo msaidia na kumshauri atakaye atayeshika madaraka.kama walivyomshauri na nchi iko shwari.