Wednesday, June 17, 2015

NG,OMBE 94 NA MBUZI 75 WA MFUGAJI MMOJA JINA LAKE HALIJAPATIKANA KATIKA MANISPAA YA DODOMA WAMESHIKWA WAKIWA SAZURULA KATIKA MANISPAA HIYO KUTOKANA NA KUKIUKA AGIZO LA SERIKALI LA KUHAMISHA MIFUGO YOTE KWENDA NJE YA MANISPAA

Uongozi wa Manispaa ya Dodoma ilishatoa agizo kuwa kila mfugaji ahamishe mifugo yake kupeleke nje ya Manispaa,na atakayekiuka agizo hilo ng,ombe akikamatwa atapaswa kumlipia shilingi 20,000 na mbuzi shilingi 10,000.kila mmoja.
Kwa hiyo mfugaji huyo anang,ombe 94 kila mmoja shilingi 20,000 sawa na shilingi 1,880,000 na mbuzi 75 ikiwamo mmoja shilingi 10,000 ,mfugaji huyo italazimu kulipa shilingi 2,630,000 kwa sababu ya kiburi na ujeuri wa kupingana na maagizo yanayotolewa na Serikali.
Mmoja anayeshughulikia mifugo inayo zurula hovyo katika Manispaa hii alisema,mara nyingi wenye mifugo wamelekezwa nini cha kufanya,lakini wanakiuka,nakwamba mjini kuwepo na mifugo inayochungwa haileti picha nzuri ni vyema watoe ushirikiano na mamlaka husika ,kuhamisha mifugo mbali na Mji.

JAJI MKUU MSTAAFU AGUSTINO STIVIN RAURENCE RAMADHANI ASEMA ANAUWEZO WA KUWA RAIS IWAPO CHAMA CHAKE KITAMPA RIDHAA YA KUONGOZA


Jaji Ramadhani aliwahikuwa askari kwa cheo cha Luteni Usu mwaka 1971 na hatimaye Brigedia Jenerali,vita vya Uganda naye alikuwemo.akaongeza kuwa mwaka 1978 alikuwa Naibu Katibu Mkuu Zanzibar.


Alisema kuwa baadaye aliteuliwa kuwa Jaji Mkuu Zanzibar na hatimaye Tanzania Bara hadi kustafu kwake,na kwamba hadi sasa ni Jaji Mkuu wa Afrika na ni Mtanzania wa kwanza kushika nafasi hiyo, hivyo kutokana nafasi yake aliyokuwa nayo anasema anauzoefu na anauwezo na sifa za kuwa Rais wa Nchi hii.Pia ni msafi hana tuhuma za rushwa.

Kuhusu mauaji ya wenye ulemavu wa ngozi ,amesema yeye akiwa Rais atahakikisha kunatolewa elimu kwa wananchi kuondoa imani potofu ya kuwa viungo vya Albino vinampa mtu utajiri au cheo nasio mwili mzima.na kwamba serikali iliyoko madarakani imeshaanza kuchukua hatua kali kwa wale waliobainika wamefanya mauaji kwa walemavu wa ngozi hao.

Aidha akiwajibu waandishi wa habari kuhusu kuwa na wafuasi wengi wakati wa kuchukua fomu, alisema .sipendi makeke wakati wa kuchukua fomu,asema kibaya chajitembeza na kizuri chajiuza.

Jaji Ramadhan amekabidhiwa fomu kadhaa zikiwemo za kupeleka mikoani kuomba wadhamini,na kisha kuzirudisha kwenye ofisi za Chama hicho Mjini hapa.

KADA MWINGINE WA CHAMA TAWALA CCM ,JAJI MKUU MSTAAFU MTUKUFU AGUSTIN STIVIN RAURENCE RAMADHANI ACHUKUA FOMU YA KUTAKA RIDHAA YA CHAMA CHAKE KUGOMBEA URAIS,KATIKA OFISI ZA CHAMA HICHO MJINI DODOMA LEO.




Jaji Mkuu Mstaafu Agostino Stivin Raurence Ramadhan akikabidhiwa baadhi ya fomu ,zikiwemo fomu za kupeleka mikoani kupata wadhami ni watakao mdhamini ,na kuzirudisha katika ofisi ya Chama Tawala CCM mjini Dodoma leo


Sunday, June 14, 2015

SEND OFF NA HARUSI HAZIWEZI KUWA NA MANJONJO BILA YA VIJANA WA SHOO, BASI HAO VIJANA MAARUFU KWA USHEREHESHAJI WA SHUGHULI HIZO HAPA DODOMA





Hawa vijana machachari sana katika Shoo kwenye Send Off na harusi mbalimbali , wanafanya maharusi na wageni waalikwa  kuona sherehe inachukua muda mfupi





Ndiyo hawa katika ukumbi wa Kilimani katika Manispaa ya Dodoma






Maharusi watarajiwa na wasimamizi wao,kushoto ni wasimamizi au wapambe na kulia ni Bwana na Bibi watarajiwa.
Hapo napo ni miondoko ya ngoma ya Kizigua ndani ya usiku wa Send off Kilimani
Mama akisema jambo upande wa wazazi wa Kiumeni

MANISPAA YA DODOMA YAWEKA MJI WAKE KATIKA HALI YA USAFI KWA KUWEKA MAPIPA YA TAKA KILA MTAA, ILA KATIKA SOKO LA SABASABA KUNA RUNDO LA TAKA ZA MAJANI YA MIGOMBA





Mapipa kama haya yapo mitaa yote katika Manispaa ya Dodoma,na kila yanapo jaa kuna magari ya kuzoa taka , yanatoa taka zile na kuacha mitaa safi.
Tofauti ipo katika masoko ya matunda na mbogamboga,Blog hii ilifika katika  moja ya soko la Sabasaba  la mboga na matunda na kushuhudia mlima wa taka taka  na pembenei kuna lori lina pakua mabaki ya taka na kuzitelekeza pale ..Huwenda Bana afya akipitia ataamuru lori la kusomba taka lifike, ili kunusuru wafanya biashara na wateja wao kunusa harufu mbaya kutoka kwenye taka hizo.

Saturday, June 13, 2015

AMANI,UVUMILIVU,UPENDO,FURAHA NI MANENO YA MZEE SEMKURUTO KWA ATHUMANI MOHAMEDI NA SUMAIA ,ALIPO WAPA MANENO YA FARAJA KATIKA MAISHA YAO YA NDOA ,KATIKA UKUMBI WA CHAMA CHA WALIMU MANISPAA YA DODOMA JANA

 Bwana na Bibi Athuman Mohamed wakifungua Muziki katika Ukumbi wa Chama cha walimu katika harusi yao jana Manispaa ya Dodoma
 Wazazi wa  Bibi Harusi Sumaia Baba na Mama mzazi
Picha ya pamoja na maharusi na kamati iliyofanikisha sherehe hiyo
 Mama mzazi wa Bwana Harusi Athumani Mohamedi
  Bw. Mnyinvua kushoto na Mzee Semkuruto mwenye tai,upande wa wazazi wa Bw.Harusi
 Bwana Harusi na Bibi harusi wakila chakula,ambapo Bibi harusi anamlisha kipande cha mguu wa kuku Mmewe mpendwa



Picha ya pamoja Maharusi ,Mama mzazi na Mwenyekiti wa Kamati kushoto

SEND OFF YA SUMAIA KATIKA UKUMBI WA KILIMANI MANISPAA YA DODOMA NA MMEWE MTARAJIWA ATHUMANI MOHAMEDI BAADA YA KUKARIBISHWA NA MWENZA WAKE

 BWANA ATHUMAN MOHAMED NA MKEWE MTARAJIWA BI.SUMAIA KATIKA UKUMBI WA KILIMANI JUZI MANISPAA YA DODOMA
BAADHI YA WAZAZI UPANDE WA BWANA ATHUMANI ,BAADA YA SEND OFF HIYO ILIFUATIA HARUSI SIKU YA PILI.