Sunday, January 5, 2014

IWAPO KUMEIBUKA HOJA YA KUWEPO KWA SERIKALI MBILI ,AMBAPO WANANCHI WENGI WANATAKA KUWEPO NA SERIKALI TATU NA HASA VIJANA WALIYOKO KWENYE VYUO MBALIMBALI, JE SERIKALI IMEJIANDAAJE KUWAELIMISHA UZURI WA KUWA NA SERIKALI MBILI NA UBAYA WA KUWA NA SERIKALI TATU?




Maswali kadhaa yanaulizwa na watu kuhusu masuala ya kuwepo   kwa Serikali mbili au tatu,na kuna vuta ni kuvute katika hoja hiyo kwa wananchi , ambapo wengi wao hasa vijana wengi wanataka kuwepo kwa Serikali tatu na ni kitu ambacho kinatarajiwa kuwepo kwenye Katiba ya Nchi.

 Sasa iwapo inatokea  kutoka kwa baadhi ya wananchi wachache wenye hoja ya kuwepo kwa Serikali mbili,wakati wengi wao wanahitaji kuwepo na Serikali tatu na hasa wasomi vijana katika vyuo vya elimu ya juu nchini.
   Ni nini unadhani kitatokea baada ya kutangaziwa hivyo? Na je iwapo itatokea hivyo Serikali imejiandaaje kutuliza au kuwaelimisha watu hao ambao wengi wao wamechoka kuwa na Serikali mbili na wanadai Serikali tatu bila kujali athari zake baadaye “ liwalo na liwe itajulikana mbele kwa mbele”
   Jambo hilo siyo la mzaha wala si la kulichukulia juu juu,kwa kuwa vijana wetu wengi bila kujali wasomi ama si wasomi,wavijijini au wa mjini wote wamekuwa na kauli moja.Hivyo Tume ya katiba iliangalie kwa macho mawili matokeo ya Hoja hiyo,na namna gani watalikabili suala hilo iwapo litatokea.Hatupendi litokee.


Friday, January 3, 2014

FAMILIA YA BWANA SIKAPUNDWA KUFANYA HAFLA FUPI YA KUMPOKEA NYUMBANI KWAKE BAADA YA KUTIMIZA MIAKA 60 TAREHE 25/13/2013 ,ILIYOFANYIKA NYUMBANI KWAKE MJINI DODOMA JANA

 Bwana Sikapundwa analishwa keki na mkewe Mrs Sikapundwa
BwSikapundwa anamkabidhi keki mkewe
 Gw.Sikapundwa anamlisha mkewe keki
 Bw. Sikapundwa anamlisha Baba Mkwe wake Mzee Bickson Bilali wa miaka 100 na siku 2
 Mr & Mrs Sikapundwa
 Bw.na Bibi Sikapundwa kushika kisu kukata keki haipo pichani
 Mama Mdogo Yunesi Mwakyusa akikata vipande vidogo keki na ndiye mtengenezaji wa keki na bingwa wa upambaji kumbi za sherehe.anapatikana karibu na majengo ya Bunge Mjini Dodoma.
 Wanamlisha keki binti yao wa Kwana Anna Sikapundwa Mwanafunzi chuo cha Biashara ASEK  Dodoma.
 Wanamlisha keki mtoto wao wa tatu mwalimu Michael Sikapundwa Manispaa ya Morogoro Mwanafunzi wa Open na Media.
Wanamlisha mtoto wao wa mwisho Bw. Emanuel Sikapundwa Dereva wa nyumbani na nimjasilia mali.
 Wanamlisha keki binti wa kwanza wa mama mdogo Mwl Mwanafunzi Mtwara Magegreth Mwakyusa
 Mama mdogo Yunes Bilal Mwakyua analishwa keki
 Wanamlisha kike mama mkwe wao Mrs Micaheli mwalimu Manispaa ya Morogoro
 Wanamlisha keki mke mtarajiwa wa Emanueli Mama Esta Mwajuma Bushiri
 Wakijiandaa kuwalisha mama wakwe zao
 Kukabidhiwa keki kwa ajili ya baadaye wakati wa mapumziko
 Kumlisha keki mtoto Sarah mwanafunzi Dodoma Seko
 Kumlisha keki mjukuu wa Maico carlen
 Mwalimu Maiko akieleza wasifu wa baba na mama yake kama MS katika hafla hiyo
 Mama Sikapundwa akisema jambo kuhusu safariya maisha yao hadi kufikia hapo wakiwa na watoto watano na wajukuu wanne.
 Picha ya Bw.na Bibi Sikapundwa na wajukuu
 Wajukuu wakisakata rumba waliloandaliwa na DJ wakiwaburudisha babu na bibi na waliyo hudhuria
Mrs,Mama Magreth Nelson Mwakyusa mtaalamu wa kutengeneza keki za ngazi zote kwa bei poa na ni mpambaji wa kumbi za sherehe anapatika kota za makole ,mkabala na majengo ya Bunge mjini Dodoma.kwa wakazi wa Dodoma na mokoa ya jirani mnaweza kupata huduma kutoka kwake.



Bwana Christian Sikapundwa amefikia umri wa miaka 60, ambapo ilipofikia tarehe 25/12/2013 ilikuwa ukomo wa Utumishi wa Umma Serikalini, akiwa mwalimu na Mhariri wa Magazeti vijijini Kanda ya Kusini.
Kwa namna ya pekee familia yake iliamua kufanya hafla fupi ya kumpokea Mstaafu huyo,ili kuungana na familia yake kwa namna moja ama nyingine ni kitendo cha kumshukuru Mungu kwa kumweka salama hadi siku ya mwisho ya kustaafu kwake akiwa na afya njema.
Hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa nyumba yake iliyojumuisha watoto wake wakiume na wake zao,watoto wakike pamoja na wajukuu wake.
Aidha pia ilimjumuisha na Baba Mkwe wake Mzee Dickson Bilali mwenye umri wa miaka mia moja na siku tatu,akiwa bado na afya nzuri na mwenye uwezo wa kusoma maandishi ya Biblia bila miwani.
Aidha mzee huyo alisema  kuwa baadhi ya vijana wa siku hizi hawawezi kufikia umri wake kwa sababu ya mabadiliko ya maisha yanayo wafanya vijana wengi kuiga matendo mbalimbali ya nchi za nje,na kwamba vyakula vingi vimekuwa na kemikali nyingi ikilinganishwa na vyakula walivyo vitumia enzi ya ujana wake.
Ili kuwapa picha halisi ya maisha ya Bwana Sikapundwa Mke wake Mrs Sikapunwa alisema neno kuhusu maisha ya Bw. Na Bibi Sikapundwa, alisema kwa niaba ya familia kuwa ili walazimu kufanya hafla hiyo kwa lengo la kumshukuru Mungu kumpa afya njema akiwa kazini hadi siku yake ya mwisho alipokabidhi ofisi.

Tuesday, December 31, 2013

HANDING OVER THE CERTIFICATE OF HAND OVER TO JUMA T, NYUMAYO





Handing over the certificate of hand over to Mr Juma T. Nyumayo as a new Editor of Southern Zone.Ruvuma,Lindi and Mtwara.

Friday, December 27, 2013

KILA CHENYE MWANZO HAKIKOSI KUWA NA MWISHO.HII NI SIKU AMBAYO ILIKUWA YA MWISHO WA UTUMISHI WANGU WA UMMA KANDA YA KUSINI







WATOTO WA SHULE YA AWALI CHARITY UWANJA WA SABASABA SONGEA WAMALIZA ELIMU YA AWALI

Mgeni Rasmi Bwana Bakule bakule maarufu kwa kuwa na timu yake ya miguu Matarawe Songea aliahidi kutoa mchango wake wa shilingi laki mbili.
Aidha alisema kuwa elimu ya Awali ni muhimu sana kwa kuinua taaluma hasa shule za English Medium,na kwamba alisema wakaze uzi wa kuendeleza watoto hao hadi darasa la saba
 Baadhi ya mwanafunzi wa Awali akimkabidhi shairi Mgeni Rasmi siku hiyo ya Awali
 Wanafunzi hao wakisoma shairi bila kubabaika utadhani darasa la saba kumbe ni watoto wa Awali

Baadhi ya wazazi wa watoto waliyo maliza elimu ya Awali siku hiyo

Thursday, December 26, 2013

Kifo cha mtoto Jems Steven wa mwaka mmoja na miezi miwili cha kinyama chashitua wakazi wa mtaa wa nanenane katika Manispaa ya Morogoro leo

Mtoto Jems Steven wa Mtaa wa Nanenane katika Manispaa ya Morogoro akutwa amekufa wakati mwili wake umefunikwa na takataka za mto Morogoro akiwa amekatwa sehemu zake za siri ,kidole na kuchomwa na kitu chenye ncha kali katika paji la uso.
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Bw. Isack Ilomo ,anaema mtoto huyo alipotea jana jioni wakati mama yake mzazi alipo mwacha akinywa uji wakati yeye alienda kuchota maji nje ya nyumba yao ya kupanga,
Alisema mama huyo baada ya kuona mwanae hayupo aliwauliza wapanagaji wenzake kama wamemwona mtoto wake ,nao walikataa kuwa hawaja mwona wala kumwona mtu aliyeingia chumbani mwake kwani ni muda mfupi tu alipo mwacha mtoto huyo.
Alipeleka taarifa kwenye uongozi wa Serikali ya mtaa,Uongozi ulikwenda kwenye kituo kidogo cha polisi kuomba kibali cha hufanya upekuzi ili kubaini kama kuna mtu alimficha kwa malengo yaliyojitokeza. Polisi walikataa kutoa kibali wakidai mpaka baada ya masaa 24 ndipo kibali kitolewe.
Baada ya masaa hayo wananchi wameukuta mwili wa mtoto huyo pembeni ya kijito cha Morogoro akiwa amekufa.Kutokana na kifo hicho cha kusikitisha kimefanya wananchi wa mtaa huo kukilaumu kituo cha polisi kwa kukataa kutoa kibali kama wananchi wa mtaa huo walivyo omba,kwani walivyokuta  maiti hiyo ilikuwa bado ina joto,ni dalili kuwa kitendo hicho kilifanywa baada ya masaa hayo 24.Ambapo ni leo.
Ifike mahali sheria nyingne za Jeshi la Polisi zilegezwe ,maana raia hawezi kufanya upekuzi wa nyumba hadi nyumba bila ya search warrant.kama wangeruhusu wangeokoa maisha ya mtoto huyo.kwa vyovyote vitendo vilifanywa na majirani palepale hasa wapangaji wenzake.
Mwili wa Mtoto huyo umesafirishwa kwenda kuzikwa kijijini kwa wazazi wake mbele ya Biahawana Mkoani Dodoma Jioni hii leo kwa mazishi.Mungu ailaze roho ya Marehemu Jems Steven mahali peme peponi Amein.

Monday, September 9, 2013

SERIKALI YAAGIZA MIKOPO YA ELIMU YA JUU IRUIDISHWE ILI WENGINE

 Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe.Dkt Shukuru Kawambwa akiongea na wahitimu wa Stashahada na Shahada ya Kompyuta Sayansi katika chuo cha St,Joseph Songea leo wanachuo 96 wamehitimu mafunzo hayo.




 Picha ya pamoja ya wahitimu wa Shahada ya kwanza katika Kompyuta Sayansi
 Picha ya pamoja ya wahitimu wa Stashahada
Picha ya pamoja ya wahitimu wa Stashahada

 Wahitimu wakila kiapo kabla hawajatunukiwa Stashahada na Shahada zao.
Mawaziri wakimsikiliza mtoa maelezo kwenye chumba cha Kompyuta sayansi



SERIKALI imewataka wanafunzi wa elimu ya juu ambao wanakopeshwa fedha na Bodi ya mikopo nchini kuirejesha mikopo hiyo,mara tu  wanapo malize elimu yao na kufanikiwa kupata ajira, kwa kulipa mikopo hiyo kuitafanya serikali kuweze kuwakopesha wanachuo wengine.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Kawambwa kwenye mahafali ya nne yaliyofanyika St, Joseph  College of Information Technology Ruhuwiko nje kidogo ya Mji wa Songea leo.
Alisema serikali inahitaji kutoa elimu ya juu kwa wanachuo wote wenye sifa na vigezo vya kujiunga na vyuo vikuu nchini,na itajitahidi kutoa mikopo kwa kadiri ya uwezo wake ingawa idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa ni wengi,kwa hiyo waliyo kopeshwa wakirejesha mikopo hiyo wanachuo wenye kuhitaji mikopo hiyo watapata.
Aidha ameto rai kwa waajiri kuonyeshe ushirikiano wao na serikali  katika kukusanya fedha hizo kwa wahitimu ambao wamewaajiri, kurejesha mikopo hiyo kwenye bodi ya mikopo.na wasipo fanya hivyo hatua kadhaa zitachukuliwa zidi yao.
Alisema serikali imetengenga shilingi trioni 1.45 kwa wanafunzi wa elimu ya juu,Wizara kupitia elimu ya juu na bodi ya mikopo imeamua kuongeza kiwango cha mkopo kwa mwanafunzi wa elimu ya hiyo.
Katika mahafali hayo wanachuo 96 wamehitimu mafunzo yao na kutunukiwa Stashahada kwa wanachuo 39  katika Fani ya Uhandisi wa Sayansi ya Kompyuta na 58 shahada ya kwanza katika Uhandisi wa Sayansi ya Kompyuta.