Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bwana Said Thabit Mwambungu aongea na wandishi wa habari ofisni kwake leo kupitia vyombo vya habari,kuwaomba wananchi kuwa na uvumilivu wakati serikali ,inafanya jitihada za kutafuta vyanzo vya matukio ya mauaji yaliyotokea siku tatu mfululizo katika Manispaa ya Songea.
Aidha ameomba ushirikiano wa uongozi wa mkoa na viongozi wa mitaa,kata na tarafa wa kuwa na ulinzi shirikishi,kwa kuwa wahalifu wanaishi nao.
Aidha alisema vifo vingi vinasadikiwa vinatokana na imani za ushirikina na uchawi basi na majambazi waningilia hapohapo katika mauaji ya watu,hivyo matembezi ya usiku kama sio ya lazima yaachwe kupisha polisi na ulinzi shirikishi ufanye kazi yake.Na kwamba indapo mtu asiyejulikana,mara moja itolewe taarifa mapema kabla uhalifu haujatokea.
Waandishi wa habari wakimsikiliza mkuu wa mkoa,alipokuwa akiwataka wananchi wasubiri serikali ifanye kazi yake kushirikiana na viongozi wa mkoa na wananchi kuhakikisha hali ya utulivu inakuwa kama awali,kufuatia maandamano ya wananchi yaliyozuiwa na polisi kwa kutumia mabomu na silaha za moto kuzuia,ambapo watu wawili wamepoteza uhai wao kutokana na majibishano ya mabomu na mawe yaliyokuwa yanatupwa na wananchi.katika manispaa ya Songea leo.
Aidha ameomba ushirikiano wa uongozi wa mkoa na viongozi wa mitaa,kata na tarafa wa kuwa na ulinzi shirikishi,kwa kuwa wahalifu wanaishi nao.
Aidha alisema vifo vingi vinasadikiwa vinatokana na imani za ushirikina na uchawi basi na majambazi waningilia hapohapo katika mauaji ya watu,hivyo matembezi ya usiku kama sio ya lazima yaachwe kupisha polisi na ulinzi shirikishi ufanye kazi yake.Na kwamba indapo mtu asiyejulikana,mara moja itolewe taarifa mapema kabla uhalifu haujatokea.
Waandishi wa habari wakimsikiliza mkuu wa mkoa,alipokuwa akiwataka wananchi wasubiri serikali ifanye kazi yake kushirikiana na viongozi wa mkoa na wananchi kuhakikisha hali ya utulivu inakuwa kama awali,kufuatia maandamano ya wananchi yaliyozuiwa na polisi kwa kutumia mabomu na silaha za moto kuzuia,ambapo watu wawili wamepoteza uhai wao kutokana na majibishano ya mabomu na mawe yaliyokuwa yanatupwa na wananchi.katika manispaa ya Songea leo.
Ofisini kwa mkuu wa mkoa wa Ruvuma akiwa na waandishi wa habari