Tuesday, April 12, 2011

KIIMFAACHO MTU KATIKA MAISHA YAKE NDICHO CHAKE TAZAMA HAWA

 Kazi ni kazi mradi inamfanya mtu aendeshe maisha yake kama kusomesha,kujenga,mavazi na chakula bila kutegemea kwa mtu mwingine kwa kuomba.
Mbwana hawa ni maarufu sana wa kuuza kuku katika soko kuu la Manispaa ya Songea,huwezi kupata kuku sehemu nyingine katika soko kuu hili la Manispaa ya Songea.

HII NDIYO MANISPAA YA SONGEA MKOA WA RUVUMA MASHIMO MTINDO MMOJA KWENYE BARABARA ZAKE

 Hapa ni eneo la standi ya mabasi yaendayo wilayani vijijini,Ambapo watu wengi wanahangaika na shughuli za kuzalisha mali kwa kujiajili wenyewe kama kijana huyo hapo akiwa na mkokoteni wake.
Hii ni barabara katikati mji wa Songea ambayo inaafadhali shuhudia ukiingia  Misufini,Majengo,Ruvuma ndipo utakapojua  ni kiasi gani mvua ilivyo haribu mazingira ya Mji huuo.

HABARI KWA UFUPI.RUSHWA IMESHAMIRI BUNDA ILI UFIKE KWA BABU LOLIONDO

Magari zaidi ya 500 ya kwama katika mji wa Bunda Mkoani Mara yanayo peleka wagonjwa kwa Babu Loliondo kwa ajili ya matibabu ama kupata Kikombe.

Hoyo ni mmoja wa watu waliokwama Bunda kwa kile kinacho ambiwa bila 150,000 gari haliwezi kupata kibali.100,000 ndio kabisa gari haliwezi kupata kibali.Ama kweli usemi usemao kufa kufana kumethibitishwa  huko Bunda.

Huyu bwana anasema rushwa imetawala kweli katika mji wa Bunda ya kutoa vibali vya magali yanayoenda Loliondo kwa Babu kupata kikombe.

Kuimarika kwa Chama ni wanachama – Kikwete

 'Hatugombani tukiondoka hapa sio mtu anaandika SMS kwa viongozi kuwa hakuelewa kitu,kila mtu alipata muda wa kutosha kuelezea alichokuwa nacho' Alisema Mwenyekiti wa CCM Dkt Jakaya Mrisho kikwete katika ukumbi wa ofisi wa chama hicho white house mjini Dodoma.

Mukama arithi mikoba ya Makamba

  Baadhi ya  wajumbe wa kamati kuu ya CCM  waliopatikana mmoja wapo ni Nape Nnauye akisoma orodha ya wajumbe wa Kamati Kuu jana White House Mjini Dodoma.
 Wajumbe wakiwa makini kumsikiliza Npe Nnauye akisoma majina ya kamati Kuu ya CCM waliopatikana baada ya Kamati Kuu ya CCM kujiuzulu.
 Mmoja wa wajumbe wa Mkutano huo.
Waziri Mkuu aliyestaafu Mhe.Edward Lowasa akiwa na Muasisi wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mzee Kingunge Ngombale Mwilu katika ukumbi wa ofisi ya Chama hicho White House wakibadilishana mawazo.


Bwana William Mkama amechaguliwa kuwa katibu mkuu wa CCM na makamu wake ni Mhe.Chiligati kuchukua nafasi za wezao waliojiuzulu nyazifa zao Juzi.

Wengine wajumbe waliochaguliwa katika Kamati kuu ya CCM ni pamoja na Lameck Nchemba,Abdullah Juma, Vuai Ali Vuai,Nape Nnauye na January Makamba.

Monday, April 11, 2011

BREAQKING NEWS ! !HELKOPTA 5 ZALIPUA MAKAZI YA LAURENT GBAGBO

Helkopta 5  zikiwemo za umaoja wa Mataifa na za Ufaransa zimelipua makazi ya rais asiyetakiwa nchini Ivory Coast Jijini Abijani hapo jana,ambapo taarifa zimeripotiwa kuwa leo  Bw.Gbagbo amekamatwa.

SAMAHANI WASOMAJI WA BLOG HII SIKUWEPO KATIKA MTANDAO KUTOKANA NA SABABU ZA KIMTANDAO

Nipo tena katika mtandao  wa Blog hii,baada ya kutatua matizo ya kimtandao uliyo jitokeza,wala sikwenda kwa babu Loliondo kupata kikombe.

Ila inapendeza kweli kwenda kumwona babu live na kupata kikombe si lazima uwe mahututi,bali ni moja ya kuhakikisha miujiza ya Mungu ya kumshushia mtu dawa bila ya kupitia maabara.

karibuni sana.