Friday, December 19, 2014

438,960 KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2015,KATIKA SHULE ZA SEKONDARI ZA SERIKALI KWA AWAMU MBILI AMBAPO AWAMU YA KWANZA ASILIMIA 97.23 NA 12,432 WAKOSA NAFASI

Naibu Waziri wa Elimu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Kassim Majaliwa alisema hayo mbele ya vyombo vya Habari hivi karibuni Jijini Dar es Saam ,na kwamba wanafunzi hao ni wale waliyopata daraja la A hadi C.
Alisema wanafunzi waliyokosa nafani katika mikoa ya Dodoma wanafunzi 9,824,Dar es Salaam wanafunzi ,1,414,Morogoro 752,Mtwara 281 na Katavi 161 kwa upungufu wa vyumba vya madarasa.
Aidha alisema kuwa wanafunzi 10,331 wamepata alama za daraja A ambapo wanafunzi 98,789 wamepata alama za daraja B,342,272 wamepata daraja C,321,939 daraja D wakati wanafunzi 18,787 daraja E.
Hatimaye Naibu Waziri huyo ameaasa wanafunzi wote kutumia fursa hiyo kwa kutumia muda wao katika kusoma,pia katoa pongezi kwa wadau wote wa elimu walio fanikisha ufanisi katika matokeo hayo kwakuonyesha alama za juu kwa wavulana ilikuwa 243 na wasichana alama  240 kati ya alama 250 kwa mwaka huu tofauti na mwaka 2013 ilikuwa alama 244.

Sunday, December 7, 2014

MHE. MBOWE ANGURUMA VIWANJA VYA BARAFU MKABALA NA UWANJA WA JAMHURI DODOMA MANISPAA UKITANGULIWA NA MAANDAMANO YA AMANI KUANZIA VIWANJA VYA DODOMA SEKONDARI WAKIGAWA VIPEPERUSHI VYENYE UJUMBE MZITO " OPERESHENI ONDOA CCM DODOMA " OCD

 Hivyo ndivyo vibwagizo vya UKAWA Kwa njia ya vipeperushi vyenye Ujumbe huo,katika harakati za kupata ushindi ndani ya Vyama vya Upinzani ,Hiyo ndiyo michezo ya Siasa.
 Ni maandamano ya Amani yaliyo anzia viwanja vya Shule ya Sekondari Dodoma kuelekea Viwanja vya Barafu Mkabala na Uwanja wa Jamhuri katika Manispaa ya Dodoma leo.
Matukio hayo ni kufuatia Maandalizi ya Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mtaa unaotarajia kufanyika nchi nzima hivi karibuni.
 Gari la Matangazo na pikipiki
 Hao ndiyo Makamanda wakiwa na Mtundiko kuashiria kwamba CCM inaondolewa Madarakani na Upinzani inashika madaraka hasa kwa ujumbe wa vipeperushi  vilivyo sambazwa Mjini hapa,Lakini ni  dalili za kujiamini.
 Hayo ni maandamano ya pikipiki ya wanachama wakiwa na bendera za CHADEMA ,CUF na nyingine kutokana na Vyama vilivyounda UKAWA
 Hapa Makamanda wakiwa wana pasha pasha mvuto kwa wananchi kusogea kwenye tukio hilo la Kihistoria kama mtangazaji alivyo kuwa akitangaza kuwa ni tukio la Kihistoria la kuitoa CCM madarakani kwa kuwapa likizo isiyo na malipo, Siasa Inapendeza masikioni.Haya kazi kwao tunawatakia mafankio mema katika safari yao ya Kuiondoa CCM kama vile imelala fo fofo.
Ni baadhi ya Viongozi.Zaidi utapata kutoka viwanja vya Barafu kwenye Magazeti na Luninga.

WAJUMBE WA BODI YA "MUTUAL GENERATION OF TANZANIA ( MGT) " IMEWAKILISHA MIRADI YAO MBELE YA WALEZI WAO MIRADI ILIYOFANYIKA NA INAYOTARAJIWA KUFANYWA KATIKA UKUMBI WA 56 KATIKA MANISPAA YA DODOMA NA MWENYEKITI WA MGT BWANA FERDINAND EMILY

 Wajumbe wa BODI ya Mutual Generation of Tanzania ( MGT ) Wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza kikao chao kifupi cha kuwakilisha Mirada iliyofanyiwa kazi na inayotarajia kufanyiwa kazi.












Mwanyekiti wa MGT Bw. Ferdinand Emily akilezea malengo ya Mutual Generation of Tanzania ( MGT ) mbele ya walezi  na wajumbe wa Shirika hilo lililoundwa na wanafunzi wa vyuo vikuu vinane Tanzania ambavyo ni Dodoma UDOM, Dar es Salaam UDSM,Chuo cha Elimu ya Biashara CBE, Makumira, Usimamizi wa Fedha  ( IFM), Mipango ( IRDP ) ,SUA na Chuo kikuu cha Jordan
 Walezi wa MGT aliyesimama na kusifu na kuelekeza juhudi za MGT ni Mkurugenzi wa AFNET Sarah D. Mwaga,wa kulia kwake ni Prof. Kalafunja Osaki wa UDOM ,wakatikati ni mwenyekiti wa MGT Bw. Ferdinand Emily , wa kushoto wake ni Bw. Christian Sikapundwa Stationery mkabala na Bohari ya Mkoa wa Dodoma na wanyuma Bi.Zaituni Said Ngwanga Kaimu Mwenyekiti MGT.
 Aliyesimama ni miongoni mwa walezi wa MGT Bi Mirium Zablon wa Sahara Media Group akiwapa moyo wa kujitoa katika kuanzisha Shirika hilo lisilo la Kiserikali la Wasomi waliohitu masomo yao na wale ambao bado wapo masomoni,akito wito kuwa wale ambao hawajajiunga na MGT wajiunge ili wajenge dhana Kujiajiri baada ya masomo yao. Ambapo mpaka sasa wajumbe waliyondani ya MGT ni zaidi ya 1000 idadi ambayo ni ndogo kulingana na idaidi ya wanafunzi wote walioko katika vyuo hivyo vinane nchini.
Wajumbe wa MGT wakisiliza kwa makini ushauri na mapendekezo yaliyokuwa yakitolewa na walezi hao moja baada ya mwingine.

MGT imeandaa mradi wa shule ya Sekondari ambayo itawapa fursa kubwa ya kufanya sekodari hiyo iweza kujiendesha yenyewe .Aidha imeanzisha mradi wa ufugaji wa kuku ambao uko tayari kinacho hitajika hapo ninamna ya kupata mtaji. Pia wameandaa miradi mingine itakayo kidhi  mahitaji ya watanzani ikiwemo ufugaji wa nyuki.


Tuesday, November 4, 2014


RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE,AHIMIZA VIJANA KUJITOKEZA KUGOMBEA NAFASI MBALIMBALI ZA UONGOZI KWA SERIKALI ZA MITAA,KWA KUWA NI SAFARI YA UWEKEZAJI WA UONGOZI KWA VIJANA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na wazee wa Mji wa Dodoma leo,baada ya kukabidhiwa Risala iliyo somwa na Katibu wa Baraza  la wazee Shekhe Abdalah Makubeli.kisha ilikabdhiwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo Balozi Job Lusinde.
Mwenyekiti wa Baraza la wazee wa mji wa Dodoma Balozi Job Lusinde amkabidhi Rais Jakaya Kikwete risala ya wazee hao iliyo mpongeza kwa ufanikishaji wa shughuli alizozifanya za maendeleo katika Awamu ya nne ya uongozi wake.


Katibu wa Baraza  la  wazee mkoa wa Dodoma Abdalah Makubeli alisoma Risala  kwa niaba yao wazee hao.
I .Walishukuru kwa kukubaliwa kuongea nao ,Aidha Risala hiyo ilielezea ( Suala la kukua kwa uchumi, kuinua uchumi Mkoani Dodoma na  taifa  kwa ujulma ,Kutuwezesha katika kilimo cha zabibu, viwanda ili kutoa ajira kwa vijana wetu.

Katika usindikaji wa mafuta ya kula na vya  nyama.  Pia walilisemea Suala la Makao makuu lipewe Msukumo  pamoja na kuiomba kuangalia Bodi ya SDA ili kusaidie ustawisishiji wa mji wa Dodoma.

Walisemea kuhusu ,muundo wa kusimamia Ardhi na makazi, na kuweka wazi ratiba ya utekelezaji na ustawisishaji wa Makao Makuu. Hivi sasa mkoa  unakuwa kwa kwasi. Mf kujengwa vyuo vikuu vikubwa katika Afrika mashariki na hivyo wameomba kuipa  Hadhi kuwa mji wa Dodoma na kwa wa  kimataifa.napia liwe  jiji.

Wamesema kwa kuwa miundombinu yake ni bora inayo kidhi mahitaji ya kuwa Jiji kama Majiji mengine nchini.

Sisi wazee tumeona upo umuhimu wa kushukuru maisha ya mama na watoto tunaomba kukamilisha ujenzi wa jingo katika Hospitali ya mkoa lililo jengwa kwa miaka 9 bila kukamilika,kwa ajili ya mama na watoto kwenye hospitali hiyo ya Rufaa ya mkoa.na kwamba wazee hao wameomba kupatiwa huduma ya afya jirani.

Sambamba na   hayo hawakusaha Kumpongeza kwa  kuanzisha mchakato wa Katiba pamoja na vikwazo vingi.vilivyojitokeza na hatimaye Katiba iliyopendekezwa akakabidhiwa,hivyo wameomba akamilishe kabla ya kuachia ngazi na kuongezea wananchi   wajitokeze kwa wingi katika kuipigia kura ya ndiyo katiba iliyopendekezwa.

 Na hatimaye Balozi Lusinde Mweyekiti wa Baraza la wazee Dodoma  alimkaribisha Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete.kuongea na wazee wa Dodoma.

Na Rais anasema.wazee mkutano huu wameitisha wenyewe.,ningekutana nanyi lakini nilikuwa na mambo mengi.Katika kujibia Risala ya wazee hao alisema atayashughulikia na kuyafuatilia yote waliyo yaomba. Yajiwemo kwa uwekezaji  wa Hoteli,Viwanda, ili kuongeza ajira kwa vijana wao. ,Ujenzi wa jingo la hospitali ya Mkoa wa Dodoma na huduma za afya kwa wazee.na uwezekano wa kuwa Dodoma kuwa Jiji.

.Ndipo alipozungumzia mambo manne muhimu

 Alisema kuwa mahusiano yetu na China ni mazuri ambapo alipokelewa vizuri sana kwa hafla maalumu ya kutimiza miaka 50 ya mahusiano ya Serikali ya Tanzania na.Serikali ya China  ambayo iliwakilishwa na  na Makamu wa Rais na hatimaya kukutana na Rais.alisema nusu karne ya mahusiano yetu yamekuwa na mafanikioa makuwa sana.

Rais aliwahimiza wananchi kujiandaa katika  uchaguzi wa Serikali za Mitaa.TAMISEMI wamesha anza    maandalizi ya kuandaa Ratiba ambazo zimeshatolewa.kwa majina ya mitaa,na Vitongiji.

Amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kwenda kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura, aidha wakati wa kupigia kura Katiba iliyopendekezwa wananchi wajitokeze kwa wingi kwenda kupiga ya ndiyo . kwa ajili ya vizazi vyetu vijavyo.
Aidha amewataka wenye sifa kujitokeza kugombea uongozi kwenye Serikali za Mitaa watu wazima,Vijana na wanawake wasibaki nyuma kujitokeze kugombea afasi hizo.

Alisema vijana wajitokeze kugombea uongozi kwa kuwa jimo wapo ya uwekezaji katika uongzi “ ni lazima tuanze safari ya uwekezaji katika uongozi” alisema Rais.

Jingine alizungumzia Katiba iliyopendekezwa,” ni Katiba iliyo kidhi  viwango vyote,ingekuwa kwenye mpira tungesema imekamilika katika Idara zote,Katiba ni nzuri” alisema.

.






Monday, November 3, 2014

VIKAO VYA BUNGE VITAANZA HAPA MJINI DODMA HAPO KESHO

Kwa mujibu wa Katibu wa Bunge kwa waandishi wa habari Mjini hapa kuwa kesho Bunge litaanza vikao vyake ambapo waheshimiwa wabunge wameanza kuingia mjini Dodoma kwa ajili ya vikao hivyo vya Bunge.

WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE INCHINI LEO WAMEANZA MITIHANI YA KUMALIZA ELIMU YA SEKONDARI

Tujifunze kusini Blog inawatakia wanafunzi wa kidato cha nne mitihani mema,Aidha inawaombea Mungu awaepushe na vishawishi vya udanganyifu wa mitihani katika kipindi chote cha mitihani yao.