Friday, June 29, 2012

SPIKA WA BUNGE MHE.ANNE MAKINDA AWAPONGEZA WABUNGE KWA KUFUATA KANUNI ZA BUNGE KWA KUPITISHA BAJETI YA WAZIRI MKUU BILA KIKWAZO KABLA YA KUHAIRISHA KIKAO CHA BUNGE HAPO JANA


BWANA JORAMU MWAIPOPO AMSHUKURU MUNGU KWA KUMWEZESHA KULITUMIKIA TAIFA KATIKA UTUMISHI WA UMMA KATIKA KITUO CHA MAGAZETI VIJIJINI KANDA YA KUSINI SONGEA

 Bwana Joram Mwaipopo mwenye bluu suti akipeana mkono na Mkuu wa Kituo kanda ya Kusini Bwana Christian Skapundwa mwenye suti rangi ya maziwa ,wa kuagana baada ya kutumikia Taifa na kufikia mwisho wa utumishi wake.
 Hapo apeana mkono wa kwaheri na mfanya kazi mwenzake Bwana John Mponda mwenye shati leupe.
 Bwana Mwaipopo apeana mkono wa kwaheri na Mkuu msaidizi wa Kituo Bwana Juma Nyumayo kwenye ofisi ya Kanda ya Kusini hapo jana,ambapo leo tarehe 30/6/2012 anastaafu kazi kwa lazima.k
 Apeana mkono wa kwaheri na mfanyakazi mwenzake Bibi Ikofu Tusekile mwenye suti nyeusi,akiwa mwenyumishi wengine tabasamu kuonyesha aliishi vizuri na watumishi wengine.
Picha ya pamoja na watumishi wa kituo hicho,Kwa umoja wao wamemtakia bwana Mwaipopo maisha mema katika kuanza maisha mapywa ya uraiani.Kwani kila mtumishi wa kada yeyote iko siku ataacha kazi.
Hii ina maana hakuna atakayedumu kazini maisha yake yote,bali itamlazimu aondoke awapishe wengine.Tinamtakia maisha mapya aendako.

BWANA JORAMU MWAIPOPO AMEAGANA NA WATUMISHI WA TUJIFUNZE KANDA YA KUSINI LEO KATIKA OFISI ZA KITUO HICHO MJINI SONGEA


Thursday, June 28, 2012

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA ASIKITISHWA KITENDO CHA KINYAMA KILICHO FANYWA NA WATU WALIYEMSHAMBULIA DAKTARI

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda ameliambia Bunge wakati akijibu maswali ya papo kwa papo kutoka kwa waheshimiwa wabunge leo ,kuwa serikali imesikitishwa na kitendo cha watu waliyehusika katika kumshambulia Daktari hadi kumsababishia maumivu katika mwili wake.
Amesema anamuombea Mungu  ili aendelee vizuri na kwamba uchunguzi unaendelea wa kupata watu waliyehusika na tukio hilo.
Kuhusu mgomo wa madaktari Pinda amesema kuwa serikali iko katika harakati za kutafuta waganga kutoka katika taasisi mbalimbali ili kuokoa maisha ya wagonjwa walioko katika hospitali ambazo madaktari wake wako katika mgomo mkiwemo Madaktari maaskari pamoja na wale waliostaafu ,wakati serikali ikifanya taratibu za suluhu kufuatia mgomo wa madaktari.

Wednesday, June 27, 2012

MADAKTARI WAMRUDIE MUNGU WAO WAACHE MGOMO MAANA WANAO ATHIRIKA NA WANANCHI WASIO NA HATIA WALA UWEZO WA KUWATIMIZIA MADAI YAO.

Wakati Daktari Jijini Dar es Salaam yuko ICU kwa kupigwa na watu wasiyejulikana, Madaktari wa hospitali ya Mkoa Songea nao wako katika mgomo baridi wagonjwa wamefurika  hosipitalini hapo bila msaada.
   Lakini hawa walikula kiapo kuwa watalitumikia taifa kwa uwezo wao wote, ambao wamechukua dhamana ya maisha ya wananchi wa nchi hii, Lakini wamesahau kuwa walikula kiapo cha utii kwa taifa.
  Pia Serikali nayo ifikie mahali iwatekelezee madaktari hao na watumishi wengine wa kada mbalimbali wanao dai maslahi yao ili kuepusha dhahama zinazotokea kwenye migomo, halafu haipendezi ni aibu kwa nchi yenye serikali sikivu  ifike mahali serikali isema sasa migomo basi,  na inawezekana.

Tuesday, June 26, 2012

OPERESHENI ya polisi Ruvuma yashika silaha 17,Risasi,madwa ya kulevya na pombe haramu.

RPC Ruvuma kamishina Msaidizi Deusdedit Nsimeki akiwaeleza waandishi wa habari mafanikio ya Operesheni iliyoendeshwa na Polisi ambayo silaha 17 zimekamatwa,risasi,pombe haramu madawa ya kulevya pamoja na wizi na unyang'anyi wa kutumia silaha na wizi.
 Kamanda akijibu hoja na mwaswali kutoka kwa waandishi.
Baadhi ya waandishi wakitafakali jinsi Operesheni kamata silaha ilivyofanikiwa.
Kamanda,Gerson Msigwa TBC katikati na Mosesi Konara kulia wakisikiliza maoni na usahuri kutoka kwa waandishi hao leo.


KAMANDA wa Polisi Mkoa Ruvuma Kamishina Msaidizi Deusdedit Nsimeki ameaambia waandishi wa habari katika ukumbi wa Polisi mkoa leo kuwa,silaha 17  zimekamatwa zikiwemo short gun  3,na  Rifle 3 magobole 11, pamoja na risasi na kesi 7 za watuhumiwa ziko mahakamani.
  Aidha Kamanda Nsimeki alisema katika Operesheni hiyo,kesi 10 zilizohusisha bangi ziko mahakamani ,pamoja na kesi za pombe haramu ya gongo lita 60.5 zilizokamatwa zilizowahusisha watuhumiwa wauzaji na wanywaji wa pombe hiyo.
    Nyingine na unyang’anyi wa kutumia nguvu kesi moja na unyang’anyi wa kutumia silaha watuhumiwa 12, kati yao 6 wapo mahakamani ,pamoja na wizi wa diseli,nondo 147  za kutengenezea madaraja, zilizosadikiwa kuibwa kwenye kampuni ujenzi wa barabara, Pia wizi wa mbuzi 7 na kesi yake ipo mahakamani ikiwa ni pamoja na uzururaji mitaani bila kazi maalumu
    Kamanda Nsimeki ametoa wito kwa wananchi wa mipakani kuacha kutumia silaha wanazozimiliki kisheria  kuazimisha kwa watu ambao hawajui matumizi yake kama ni ya uahalifu au la.Alisema zoezi la kusaka silaha zinazotumiwa kinyume cha sheria linaendelea ikiwa ni zoezi endelevu.

Thursday, June 21, 2012

Serikali mkoani Ruvuma inampango wa kuwakopesha wakulima ili waachane na jembe la mkono

Bwana Mwambungu amewaambia waandishi wa habari kuwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma ni wazalishaji wazuri wa zao la mahindi kwa kutumia jembe la mkono,na kama watatumia Matrekta na kuliacha jembe la mkono wazalisha mara dufu.
Kwa hiyo Serikali ya Mkoa huo itawapelekea wananchi matrekta ya kukopesha wakulima,maana msimu huu mahindi ni mengi yatauzwa na kubakia na ziada kwa chakula chao ,mkoa umetimiza kaulimbiu ya kilimo kwanza kwa vitendo.

Sunday, June 17, 2012

SALAAM ZA JUMAPILI KWA WATUMIJI WA MITANDANO YA KIJAMII MATUKIO YA MKOA WA LINDI

 Kijana huyo anaonekana akiendesha naiskeli kwenye mchanga pembeni mwa bahari,ni miongoni mwa akazi wa Mji wa Lindi Jioni kubaridhi kando ya bahari wakipunda upepo.
 Lakini wanapo kuwapo wenyeji na wageni hawakosikani basi siku hiyo nami pia nilipata muda wa kwenda kwenye bandari ya Mkoa wa Lindi ambayo sikuhizi haifanyikazi kama zamani.
 Asubuhi moja baada ya kumaliza shughuli Kilwa Masoko,tulikuwa tukijiandaa kwenda kilwa Kivinje kuendelea na shughuli zetu,kama unavyo Bwana Juma Nyumayo akiwa na begi lake tayari kuelekea standi ya mabasi hapo Kilwa Masoko.
 Hiyo ndiyo madhari ya ufukwe wa Pwani ya Lindi na vivutio vya Mikoko,ambayo imeenea Pwani yote ya Mwambao mwa Bahari ya Hindi.
 Wakazi wa Kilwa Masoko,Kisiwani na hata kilwa Kivinje ni wavuvi,Bwana Juma nyumayo anaonyeshwa na mvuvi wa Kilwa Masoko samaki  katika soko lao ambaye anauzwa kwa shilingi 20 elfu.
Hapo ni shamba la kutengeneza chumvi  yenye madini ya joto.  mkoani Lindi,ni aina ya ajira wanchi hao wamejiajiri kwenye ukusanyaji wa chuchi.

m


Thursday, June 14, 2012

VIONGOZI NA WATENDAJI WAWAJIBIKE KIKAMILIFU KWA WANANCHI –MKUU WA WILAYA YA SONGEA

 Mkuu wa Wilaya ya Songea Bwana Joeph Joseph Mkirikiti akizungumza na waandhi wa habari ofisni kwake leo.Mjini Songea.
 Bwana Mkirikiti akiwaonyesha waandishi wa habari daftari la wakulima wa Manispaa ya Songe Mjini Magharibi lililo andaliwa na Mkuu wa Wilaya aliyestaafu Bw.Thomas Sabaya.na yeye anaanda dafutari la wafanya biashara wa manispaa ya Songea.
Waandishi wa habari wakiwa ofisini kwa mkuu wa Wilaya wakimsikiliza mikakati aliyoiweka ya viongozi na waendaji kuwajibika,maana uwajibikaji ni ngao ya maendeleo ya wananchi.
Waandishi wako makini kumsikiliza mkuu huyo leo ofisini kwake.





MKUU wa Wilaya ya Songea Bwana Joseph Joseph Mkirikiti ametoa rai kwa viongozi na Watendaji wa Serikali kuwajibika kikamilifu kwa wananchi ambao wao wanawalipia mishahara,na kwamba waache kufanya kazi kwa mazoea.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake ambao leo kuwa  rai hiyo ameshaitoa kwa watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea na Halmashauri ya Songea Vijijini na hatimaye ataongea na waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri zote mbili za Halmashauri ya Manispaa ya Songea na Halmashauri ya Wilaya ya Songea Vijijini..
         Bw.Mkirikiti alisema kuwa  wananchi wa Manispaa,Songea Vijijini na Mkoa mzima kwa jumla watumie fursa zilizopo katika kuwaondolea umasikini wa kipato kwani kutokana na takwimu za mkoa mwaka 2006 ,kipato cha mwananchi wa Songea ni Tshs, 156,000/= kwa mwaka.ambacho hakitoshelezi mahitaji ya mwanachi huyo.
        Aidha alisema wakitumia fursa hizo watazalisha zaidi watauza mazao yao ambapo watapata fedha zitakazo inua misha yao.Na kwamba yote hayo hayawezi kufanikiwa iwapo uwajibikaji utakuwa haufanyiki kikamilifu.
       Kutokana na hilo mkuu huyo amewsihi  watendaji hao wawajibike kwa wananchi katika kujibia kero zao  mbalimbali zikiwemo zinazohusiana na ardhi na wala wasigeuke kuwa madalali wa ardhi.
    Kuhusu changamoto zilizopo katika Wilaya zake, alisema zimeshaanza kushughulikiwa zikiwemo za umeme, ambao ulikuwa haueleweki vizuri lakini sasa upo katika hali nzuri,lakini alichokiona kuwa ni tatizo la uwajibikaji kwa watendaji wa “Tanesco” wa kufanya kazi kwa mazoea.
     Ametoa wito kwa vijana kutumia fursa ya Boda ya Msumbiji kwa kufanya biashara za mipakani,na kufanya bishara zao ndogondogo katika maeneo yaliyoruhusiwa badala ya kupanga barabarani na kuwa kero katika Manispaa.


Wednesday, June 13, 2012

HIVYO NI KWELI ? AKINA MAMA WANAMOYO MGUMU HIVYO? TAFAKARI!

Wewe na mie tuchunguze vizuri photo hiyo, ni dampo la takataka eneo moja huko Mtwara,lakini ukichunguza sana utaona ni uchafu uliyokuwa pamoja na binadamu,binadamu aliyezaliwa na mwanamke.
Ni kitoto kichanga kilichozaliwa na mama huko Mtwara na kukitupa kwenye lindi la mikusanyiko ya kila aina ya uchafu,Hivyo wimbo wa nani kama mama una maana yoyote kwa akina mama wenye moyo wa ukatili kama huyo? .je ni kitu gani kilicho msibu mama huyo hadi kufikia kufanya kitendo hicho kiovu.( Source Mitandao ya Kijamii ).

Saturday, June 9, 2012

SAFARI HII YA KIKAZI LINDI NA MTWARA NIMEJIFUNZA MENGI.

 Wenyeji wa Mji wa Lindi wanajishughulisha na ukusanyaji wa chumvi na kuiwekea mqdini joto,wajipatia kipato kutokana na kazi hiyo.
 Jioni nilikuwa natokea zangu bandarini Lindi mjini kuona jinsi majengo ya bandari hiyo yalivyo telekezwa
Hilo nalo ni eneo jingine ambalo chumvi inakusanywa na wakazi hao wa Mji wa Lindi,chumvi ambayo soko lake liko Dar es Salaam.
 Huyo na Mwanataaluma wa habari Kanda ya Kusini katika shughuli za kikazi Mtwara na Lindi Bw.Juma Nyumayo akiwa anaondoka kutoka Kilwa Masoko na Kuelekea Kilwa Kivijne kuendelea na shughuli hivi karibuni.
Hizo na ofisi za Bandari ya Lindi ambayo imetelekezwa,haifanyi kazi kama mwanzo ambapo meli zilikuwa zikitia nanga katika bandari hiyo.
Hilo na baadhi ya majengo yaliyojengwa enzi ya utawala wa kisultani mwambao wa Pwani ya Afrika mashariki,Hiyo miti siyo mapambo bali ni miti iliyoota ndani ya jengo na kubomoa kuta zake,Utalii usisubili wazungu kuja kuoana maajabu ya kale,na jinsi babu zetu walivyo weza kujenga majumba bila ya kutumia sementi au tofali.
 Nilikuwa nashangaa kuona mchanga ulivyo jaa kwenye eneo ambapo meli zilikuwa zikitia nanga enzi zake za MV Lindi ikitamba baharini siku mbili kutoka Dar es Salaam hadi Lindi,Tiketi unaisotea wiki mbili kwa bei ya halali Mlango wa nyuma siku moja au mbili unasafiri,Hizo hapo ni meli ambazo zinakarabatiwa ziludishwe Zanzibar.
 Pwani ya Lindi jioni watu wanapunga upepo
Wengine wanaogelea,wanacheza basi mradi wanajiburudisha kwenye bahari ya maji ua chumvi,hiyo ndiyo safari yetu na Bw.Nyumayo mikoa ya Mtwara na Lindi tutaendelea kipindi kijacho.

MKOROSHO UKITUNZWA VIZURI UNATOA MAZAO MENGI,WAKULIMA WA ZAO HILO KATIKA MIKOA YA RUVUMA,MTWARA NA LINDI WAMEHAKIKISHIWA SOKO LA UHAKIKA WA ZAO HILO

 Korosho ilipaliliwa inapendeza licha ya kuwa zao la bishara,shamba kama hilo lililoko Wilaya ya Lindi vijijini ni safi,pia hata uokotaji wa korosho zilizodondoka na rahisi,pia hata matunda yake " mabibo' wenyeji wa mikoa ya Mtwara huwa wanatengeneza pombe ya mambibo wanayoiita Uraka.
Walanguzi waliingilia soko la zao hilo kwa kasi kwa wakulima ambapo waliuuza korosho zao kwa bei ya hasara kwa sababu ya shida za wakulima wa zao hilo,lakini sasa Serikali imetoa angalizo kwa walanguzi na wakulia wapelekekorosho zao kwenye vyama vya Ushirika.

Sunday, June 3, 2012

HAPA KWETU SHEREHE NI CHAKULA'SHEREHE KULYA' MAMBO HAYO

 Msosi wa nguvu ulikuwa unapakuliwa tayari kwenda kwa kamwali Evaristi Jahazi na wapambe wake baada ya kumzawadia au kufupa.ni msosi kwelikweli .
Baadhi ya akina mama wakishuhudia tendo la kufupa na kurudisha MAJAMANDA kwa mama wa mtoto huyo ambayo yeye alikuwa akiwapa wenzake kwa shughuli kama hizo."Chama kiuyai" By Nguni People.


Mama kulia Evaristo katika na kaka Zenobius Matembo kushoto wakiwa nyumbani jana baada ya kutoka kanisani.

JANA MANISPAA YA SONGEA MKOA WA RUVUMA WATOTO WALIPATA KOMONIO YA KWANZA EVARISTO JAHAZI ALIKUWA MMOJA WAO

 Evaristo Jahazi mwanafunzi wa darasa la nne katika shule ya msingi Mwembe chai Manispaa ya Songea Jana alipata Komoni ya kwanza katika Imani ya Kanisa Katoliki la Mitume.Amependeza na amefurahi kuingia katika hatua ya pili ya Imani ya Kumkiri Kristo.
 Hapo Evaristo akiwa na kaka yake Zenobius Matembo baada ya lutoka kanisani jana katika kanisa dogo la Matarawe Songea ambapo alipopatia Sakramenti hiyo ya kwanza.







Hapo ametulia  Bwana Evaristo.

KUNA KITU KIKUBWA KATIKA NGAO YA TAIFA

Hilo ni fumbo kubwa kwa watanzania ni Nembo inayo pendeza lakini ni ya kuichunguza na kuifahamu vyema.Ikienda sambamba na Ujumbe wake 'UHURU NA UMOJA' laiti kama watu wangelewa umuhimu wa Ngao ya Taifa na fumbo lake sidhani kama kungetokea baadha ya watu kuukataa umoja,Umoja huo ndiyo unatufanya tunaitwa watanzani 'wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania' Bila ya hivyo kutakuwa na Watanganyika,Wazanzibar na waPemba,Ambao wajaa Dar au Bongo ( Bara )
Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere aliona mbali,na akakibuni kitu ambacho kina fumbo kubwa sana ,lakini kinapendeza na kuvutia Wa - Tanzania lakini sasa kinachukuliwa kinyume na matakwa ya Mwasisi huyo.

Utatu wa Roho Mtakati ni Umoja kwa imani ya Kanisa katoliki la Mitume Ilikuwa Jumapili ua jana

 Utatu Mtakatifu ni fumbo la Imani kwa waumini wa Kanisa Katoliki la Mitume,Utatu huo ni wa Baba,Mwana na Roho Mtakatifu.Ni Umoja katika Fumbo hilo Padre Otieno anasema Dunia inakubwa na jamii inayo kosa umoja ndani yao,ndiyo maana kuna matukio ya kila mara ambayo haya mpendezi Mungu.
 Hiyo ilikuwa ibada ya Kwanza katika mfululizo wa misa zinazo pangwa kila Jumapili katika Kanisa Kuu la Mathiasi Mulumba Kalemba la Jimbo kuu la Songea.
Padri huyo katika akifukiza ubani kwenye Altare Jimboni hapo jana,katika ibada ya Fumbo hilo.